Kabla
mfugaji hajafikiria kuhusu makazi ya ng’ombe wake, ni vyema sana
kujiuliza ni kiasi gani cha mifugo utahitaji kuwa nao baada ya miaka
kadhaa hivyo kukuwezesha kutenga nafasi ya kutosha kwa ajili ya mifugo
utakayoleta.
Njia rahisi ya kulitambua hilo, ni
kujiuliza ni kiasi gani cha mifugo ungependa kuwa nao baadaye na ni
kiwango gani cha uzalishaji wa maziwa ungetarajia kufikisha kutoka kwa
ng’ombe wako.
Swali la kwanza, ni muhimu sana kwa mfugaji kujiuliza, kwani kiwango cha mifugo hutokana na uwezo wa kiwango cha lishe utakachohitajika kulisha mara kwa mara. Kwa kawaida, ekari moja ya ardhi hutoshea kulisha ng’ombe wa maziwa aina ya Freshiani mmoja au Jesrey wawili tu.
Ng’ombe wa maziwa mmoja (Fresian, Guernsey, Jersey)
kiasi cha tani 5 ya lishe ya majani mabichi au majani makavu kwa mwaka.
Hii ni sawa na kilogramu 25,000 za matete au kiasi cha majani
uliyoyaotesha kwenye ekari moja. Pamoja na usimamizi mzuri wa malisho ya
nyasi, au mchanganyiko wa malisho kama mikunde au mimea kama desmodium, ni dhahiri kuwa bado utahitajika kuwa na angalau ekari ya ziada 0.75 ya eneo ili kuweza kulisha ng’ombe wako vizuri.
Kwa ujumla, ng’ombe wa maziwa huhitaji
lishe kiwango kikubwa kuliko ng’ombe wa nyama, na mara nyingi huwa na
uzalishaji mkubwa pale ambapo ubora wa lishe ni wa hali ya juu. Hali
kadhalika, kama utazalisha malisho yako mwenyewe, bado utahitaji njia
nyingine ya ziada ya kupata lishe ikiwa itatokea tatizo lolote katika
malisho.
Jedwahi hili huonesha kiwango cha lishe
kinachohitajika kwa aina mbalimbali ya ng’ombe wa maziwa, pamoja na
ardhi kwa ajili ya kuzalishia malisho.
Ufugaji wa ndani
Katika ufugaji wa ndani, ng’ombe
wanahitajika kuwekwa kwenye hali ya usafi, na makazi yao yawe na ulinzi
wa kutosha na yenye kuwapatia uhuru. Wafugaji walio wengi wamekuwa
wakiwekeza fedha nyingi katika kuwajengea mifugo, na mwishoni kuishia
kukosa fedha kwa ajili ya kulishia
mifugo hiyo. Mfugaji anayeanza, anashauriwa kujengea mifugo yake makazi
mazuri na ya gharama nafuu na baadaye kuendeleza mabanda hayo kutokana
na mapato yanayopatikana.
Mambo ya kuzingatia katika ujenzi wa mabanda
Nafasi: Ng’ombe mkubwa anahitaji
kuwa na nafasi ya kutosha kwa ajili ya chakula, kupumzika pamoja kufanya
mazoezi jambo ambalo wafugaji walio wengi hawazingatii na badala yake
huweka mifugo yao katika nafasi ndogo ambayo mwishoni hudidimiza ukuaji
wa mnyama na uzalishaji kwa ujumla. Kwa mantiki hiyo, ng’ombe mmoja
mkubwa anahitaji mita za mraba 8 mbali na eneo lake la kupumzikia. Njia
rahisi ni kutenga eneo hili mbele ya zizi/banda. Kumbuka, unapokuwa na
nafasi kubwa, ndipo unapotengeneza uzalishaji mzuri.
Paa: Ni vyema kukawa na paa kwa
ajili ya kuilinda mifugo dhidi ya upepo, mvua pamoja na jua kali.
Hakikisha paa linakuwa juu, ili kuipa uhuru mifugo yako kutembea ndani
ya banda bila tatizo lolote. Hakikisha mteremko wa paa hauwezi kuathiri
sehemu ya mifugo kupumzika na sehemu ya lishe hasa kwa kuruhusu maji
kuingia katika sehemu hizo.
Sakafu: Hakikisha sakafu inakuwa
na mfumo mzuri wa mifereji kwa ajili ya kuruhusu maji na mkojo kupita
hivyo kuwaweka mifugo katika hali nzuri. Unaweza kutengeneza sakafu ya
simenti ambayo ni rahisi kusafisha. Hata hivyo kwa kuwa inagharimu
fedha, mfugaji anaeanza, anaweza kutumia udongo wa mfinyanzi au aina
nyingine ya udongo mgumu kutengeneza sakafu. Endapo utasakafu banda,
sakafu isiwe inayoteleza kwa kuwa ng’ombe wanaweza kuteleza na kuumia.
Sakafu iwe na mwinuko kidogo na mwinuko uelekee sehemu ya kutiririshia
mkojo na kutolea kinyesi.
Matandiko: Eneo ambalo mifugo
hupumzikia, ni vyema kukawa na matandiko. Unaweza kutumia malighafi ya
aina yeyote kavu ambayo huweza kunyonya mkojo na samadi. Matandiko hayo
ni lazima kubadilishwa mara kwa mara.
Vihondi vya maji na chakula:
Hakikisha kuna vihondi vya kutosha kwa ajili ya chakula na maji. Mabanda
ni vyema yakawa karibu na vyanzo vya upatikanaji wa maji safi na
salama. Kwa wastani, ng’ombe mmoja anahitaji kunywa maji kiasi cha lita
kati ya 50 au 80 kwa siku sawa na ndoo 5 hadi 8 za maji (za ujazo wa
lita 10).
Shimo la mbolea: Mifugo
inayolishwa vizuri hutoa samadi nyingi hivyo huweza kuwa tatizo kwa watu
wanaokuzunguka hasa ikiwa inatapakaa kila mahali na kusababisha kuwepo
kwa harufu mbaya. Kama utafuga mifugo mingi katika eneo dogo bila kuwa
na sehemu maalumu ya kuweka mbolea inayotokana na mifugo hiyo, basi ni
dhahiri kuwa utasababisha kutokuelewana na majirani, lakini pia
kutasababishia wanyama kukaa katika hali ya usumbufu. Ni vyema kuandaa
shimo maalumu kwa ajili ya samadi hasa kwa ufugaji wa ndani, kabla ya
kutumia kwa ajili ya kuweka kwenye mashamba ya malisho.
Bet on esports - Dr.MD
ReplyDeleteBet on esports by Dr.MD in 광양 출장안마 the UK and Ireland. Learn about esports 논산 출장샵 betting, 동해 출장샵 including 전라북도 출장마사지 live streams, odds, and how to deposit. 강릉 출장안마 Rating: 4.4 · 14 reviews